1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

WASHINGTON: Marekani imeashiria kundosha vikwazo

3 Machi 2007
https://p.dw.com/p/CCMn

Serikali ya Marekani inataka kuondosha baadhi ya vikwazo vya uchumi vilivyowekwa dhidi ya Korea ya Kaskazini.Duru rasmi mjini Washington zimeashiria kuwa juma lijalo,wizara ya fedha ya Marekani huenda ikatoa taarifa kuhusu suala hilo.Hatua ya kuondosha sehemu ya vikwazo,humaanisha kuwa akaunti za Korea ya Kaskazini zilizozuiliwa zikiwa na kati ya Dola milioni 8 na milioni 12 zitaweza kuachiliwa huru.