1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUkraine

Utoaji umeme kwa mgao wawaathiri mamilioni ya Waukraine

10 Novemba 2025

Mamlaka nchini Ukraine zimesema mamilioni ya watu nchini humo, wameathiriwa Jumatatu kwa kukosa umeme.

https://p.dw.com/p/53MvN
Ukraine | Ukarabati wa majengo yaliyoharibiwa kwenye mashambulizi ya Urusi
Mashambulizi ya Urusi yanayolenga miundo mbinu ya nishati ya Ukraine yawaacha mamilioni ya Waukraine taabaniPicha: DW

Hali hiyo imejiri baada ya Urusi kushambulia miundo mbinu ya nishati mwishoni mwa wiki.

Kampuni ya taifa ya umeme nchini Ukraine Ukrenergo, imetangaza Jumatatu kuwa kutakuwa na mgao wa umeme wa saa kadhaa katika maeneo mbalimbali, kutokana na mzozo wa Urusi na Ukraine ambapo vikosi vya Urusi, vilishambulia vituo vya nishati kuelekea majira ya baridi kali.

Katika tukio jingine, shirika la Ukraine la kupambana na ufisadi limesema linafanya operesheni kubwa ya kufichua ufisadi katika sekta ya nishati ya nchi hiyo.

Shirika hilo limesema wamerekodi matukio makubwa ya uhalifu na kwamba uchunguzi huo ulishirikisha saa 1,000 za sauti zilizorekodiwa kwa kipindi cha miezi 15.