1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ushoga katika michezo, kuna hofu ya wachezaji kujitokeza hadharani

Sekione Kitojo4 Agosti 2010

Wanamichezo wengi wanashindwa kujitokeza hadharani na kujitambilisha kuwa wao wanahusiana kimapenzi na watu wa jinsia sawa.

https://p.dw.com/p/Oc7O
Wanamichezo kutoka Mexico. Huo ni wakati wa ufunguzi wa michezo ya watu wanaohusiana kimapenzi na watu wa jinsia sawa , mashindano yanayofanyika mjini Koln.Picha: DW/Nelioubin

Wanamichezo  wengi   wanashindwa  kujitokeza  hadharani na  kujitambulisha   kuwa  wao  wanahusiana  kimapenzi na  watu  wa  jinsia   zao. Wanamichezo  hao  hujizuwia sana  kila  mara   hasa  inapotokea   kuwa   amepata mafanikio  makubwa   katika  michezo. Kabla  ya  hapo kunakuwa  tu  na  uvumi.

Kwa  Gareth  Thomas  hali  sio  rahisi. Kijana  huyu mwenye  mwili  uliojengeka  vizuri  kimichezo  mwenye uzito  wa  karibu  kilo  100  na  urefu  wa  mita  1  na centimeta  91, mwili  wake   unatoa  ishara.  Napambana hadi  mwisho. Katika  mchezo  anaoshiriki  wa  rugby  , yeye  ni  shujaa,  na  akiwa  ameshiriki  mara  100  katika timu  ya  taifa ni  mchezaji  anayeshika  rekodi  kuitumikia timu  ya  taifa   ya  Wales. Kwa  muda  wa  miaka  15 amekuwa  akijulikana   kuwa  ni  mchezaji   mkakamavu  na mwenye   mabavu   duniani,  na  hakuna  mtu  aliyedhani kuwa  anasiri  anayeficha. Thomas  ameweka  wazi  hali yake  hiyo , akiwa  bado  ni  mchezaji  maarufu. Ndoa  yake ilivunjika, lakini   wenzake  katika  timu  wanasema, kwetu sisi  ni  sawa  tu.  Na  kwa  hiyo  Thomas  anamtaka  kila mchezaji, hatimaye, aseme  ukweli  juu  ya  maisha  yake, na  mzigo  mkubwa   atakuwa  ameutua.

Lakini  hadi  sasa  bado  ni  wanamichezo  wachache waliochukua   hatua  kama  yake.  Hofu  ni  kubwa  mno kwa  jinsi  wezao  watakavyowachukulia, wale  wanaopinga, pamoja  na  mashabiki  wao. Katika  michezo  ya  kulipwa, suala  hili  linahusu  pia  malipo, hususan katika   mikataba ya  wadhamini. Michael  Lohaus , rais  mwenza  wa michezo  ya  watu  wanaofanya  mapenzi  na  watu  wa jinsia  sawa  mjini  Kolon , anafahamu  maamuzi  ya makampuni  makubwa.

Nimekuwa  nikisikia  kila  mara  kutoka  makampuni yanayotoa  udhamini  kuwa  watu  wanaofanya  mapenzi na  jinsia  sawa hawaruhusiwi  kutumia  huduma  zetu. Huo ndio  utaratibu  uliopo  na  Kwa  mujibu  wa  hayo  hakuna mtu  anayehitaji  mwanamume  anayehusiana  kimapenzi na  mwanamume  mwenzake  ama  mwanamke anayehusiana  kimapenzi  na  mwanamke  mwenzake kufanya  matangazo  ya  biashara  kwa  kampuni  kama hizo.

Na  inaonekana wakati  wote  kuwa  ni  tatizo  kwa mwanamichezo  kuwa  na  uhusiano  wa  kimapenzi  na mtu  wa  jinsia  yake, ambapo  katika  eneo  lingine  la kijamii  kama  siasa  ama  utamaduni , mapenzi  baina  ya watu  wa  jinsia  moja  sio  tena  kitu  cha  ajabu. Kwa Herbert  Potthoff  kutoka  katika  kituo  cha  historia  ya mashoga  kuna  hali  wakati   wote  ya  chuki  bila  sababu na  hofu  ya   kujitokeza  hadharani.

Katika  michezo  ya  kulipwa  ama  michezo  mbali  mbali hali  bado   iko  hivyo, kwamba  karibu  hakuna  mtu aliyeweza  kujitokeza  hadharani. Soka  ndio  mchezo ambao  unaweza  kupigiwa  mfano  zaidi. Hakuna  mtu anayeweza  kujitokeza. Na  hii  inahusu  hata   michezo mingine.

Ugumu  pia  anauona  Ingrid  Blom  kutoka  katika  klabu kubwa  kabisa  ya  wanawake  wanaofanya  mapenzi  na wenzao  wa  jinsia  moja  ya  Janus SC  mjini  Koln. Anasema  kuwa  michezo  ni  chombo  muhimu kinacholeta  hofu  na  kujenga  hali  ya  kujificha.

Hii  haihusiani  na  mwelekeo  wa  matamanio  yangu kimapenzi, hii  inahusu  kile  ninachoweza  kukifanya. Ni vile  jinsi  mtu  anavyoweza  kushirikiana  na  wenzake katika  timu   na  kufikia  mafanikio.

Baadhi  ya  wanamichezo  wameweza   kujitokeza. Hususan  Judith Arndt,  mshindi  wa  medali  ya  fedha katika  mchezo  wa  kuendesha  baiskeli  katika  michezo ya  Olimpiki  mwaka  2004,  ama  mchezaji  wa  tennis Gottfried  von Cramm, pamoja  na  wachezaji  wengi  wa mchezo  wa  kuteleza  katika  bafaru. Na  pia  rais  wa shirikisho  la  kandanda  nchini  Ujerumani,  DFB,  Theo Zwanziger,  anapinga  sana  chuki  dhidi  ya  watu wanaofanya  mapenzi na  watu  wa  jinsia  sawa  katika mchezo  wa  kandanda.

Mwandishi : Olivia Fritz / ZR / Sekione  Kitojo       

Mhariri : Othman  Miraji.