1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Migogoro

Urusi yazidungua droni 235 za Ukraine

14 Desemba 2025

Urusi imesema imefanikiwa kuzidungua droni 235 za Ukraine zilizolenga kuishambulia usiku wa kuamkia Jumapili 14.12.2025. Hayo ni kulingana na taarifa iliyotolewa na Wizara ya ulinzi ya taifa hilo.

https://p.dw.com/p/55K1O
Sergiyev Posad, Urusi 04.07.2025
Mlipuko baada ya moja ya mashambulizi ya Ukraine dhidi ya Urusi nje kidgo ya mji wa Moscow.Picha: Social Media via REUTERS

Gavana wa Mkoa wa Volgograd amesema ghala la mafuta katika eneo lake liliwaka moto baada ya mabaki ya droni moja iliyodunguliwa kuanguka na kusababisha mlipuko.

Safari za ndege zasitishwa kwa muda

Mamlaka ya udhibiti wa anga nchini humo imesema pia takriban viwanja kumi vya ndege vikiwemo vya Moscow na Saint Petersburg vilitangaza kusitisha safari kwa muda usiku.

Hayo yanaendelea wakati ambapo Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky amethibitisha kuwa atahudhuria mazungumzo mjini Berlin yanayolenga kuvimaliza vita nchini mwake. Mjumbe Maalum wa Marekani Steve Witkoff anatarajiwa kuhudhuria majadiliano hayo lakini Urusi haitakuwa na muwakilishi.