Trump ataka jumuiya ya NATO imkabidhi Greenland
21 Januari 2026
Rais Donald Trump ameinadi nchi yake kwamba ndio pekee yenye uwezo duniani wa kuihakikishia usalama Greenland, akidai hakuna mshirika yoyote wa Jumuiya ya Nato anayeweza kukilinda kisiwa hicho cha barafu isipokuwa Marekani:
''Nawaheshimu sana watu wa Greenland na watu wa Denmark. Lakini kila mshirika wa NATO ana wajibu wa kuwa na uwezo wa kujilinda lakini ukweli ni kwamba hakuna nchi moja wala kundi la nchi zilizokuwa kwenye nafasi ya kuweza kuilinda Greenland isipokuwa Marekani.Ni nchi yenye nguvu na tuna nguvu kuliko watu wanavyoelewa.''
Utawala wa Trump watishia kuvunjika kwa uhusiano wa Atlantiki
Akizungumza mbele ya Jukwaa la kiuchumi duniani Trump ameitisha mkutano wa haraka kuhusu azma hiyo ya Marekani ya kukitwaa kisiwa hicho chenye kujitawala ambacho ni sehemu ya Denmark, nchi mwanachama wa Jumuiya ya mfungamano wa kijeshi wa NATO ambao ameukosowa akisema hauna faida yoyote kwa Marekani. Greenland
Rais huyo wa Marekani ambaye anakosolewa na viongozi wa Ulaya amewashambulia akisema Ulaya haina mwelekeo mzuri.