1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAsia

Taiwan yasema ni taifa "huru" baada ya onyo la Trump

Saleh Mwanamilongo
16 Mei 2026

Msemaji wa Rais wa Taiwan Lai Ching-te, Karen Kuo, alisema vitisho vinavyoongezeka vya kijeshi kutoka China ndiyo “sababu kuu ya kuvuruga” utulivu katika eneo la Indo-Pasifiki.

https://p.dw.com/p/5Dppt
Eswatini Sikhuphe 2026 | Rais wa Taiwan Lai Ching-te anapokelewa na Waziri Mkuu Dlamini
Taiwan inamshukuru Trump kwa msaada wake wa muda mrefu na unaoendelea kwa usalama katika Mlango wa Taiwan, na Taipei inaendelea kuimarisha ushirikiano wake na WashingtonPicha: Taiwan Presidential Office/AFP

Taiwan imesema ni taifa huru na la kidemokrasia, saa chache baada ya Rais wa Marekani Donald Trump kukionya kisiwa hicho dhidi ya kutangaza rasmi uhuru wake kutoka China. Kauli hiyo imekuja baada ya Trump kumaliza ziara nchini China, ambapo Rais Xi Jinping alimhimiza kutoiunga mkono Taiwan.

Wizara ya mambo ya nje ya Taiwan imesema taifa hilo haliko chini ya Jamhuri ya Watu wa China na kwamba mauzo ya silaha kutoka Marekani ni sehemu ya makubaliano ya usalama kati ya pande hizo mbili.

Trump amesema hataki kuona vita vikizuka kuhusu Taiwan na amezitaka Taiwan na China "kupunguza mvutano". China inaiona Taiwan kama sehemu ya eneo lake na imekuwa ikiongeza shinikizo la kijeshi katika miaka ya karibuni.