Migogoro
Papa Leo XIV, Mahmoud Abbas wajadili hali Mashariki ya kati
6 Novemba 2025
Matangazo
Vatican imesema pande zote mbili zilikubaliana kwamba mzozo katika eneo hilo unaweza kumalizwa kupitia suluhu ya madola mawili yaani Palestina na Israel. Mkutano huo ni wa kwanza wa ana kwa ana kati ya Papa Leo na Abbas.
Umuhimu wa misaada ya kiutu waangaziwa
Wawili hao pia wamejadili hali katika Ukanda wa Gaza na kukubaliana kuhusu umuhimu wa kupelekwa misaada ya kiutu. Mahmoud Abbas, aliwahi kukutana na mtangulizi wa Papa Leo, Papa Francis mwezi Desemba mwaka uliopita.
Alichaguliwa kuwa kiongozi wa mamlaka hiyo mwaka 2005. Mamlaka hiyo inaendesha sehemu inayokaliwa kimabavu na Israel ya Ukingo wa Magharibi, lakini ikapoteza udhibiti wa Ukanda wa Gaza, wakati Hamas walipoudhibiti mwaka 2007.