1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

New York. Leo ni siku ya ukimwi duniani.

1 Desemba 2006
https://p.dw.com/p/CCni

Siku ya ukimwi duniani inaadhimishwa duniani kote leo wakati ugonjwa huo ukiendelea kuleta maafa, na watu wanaokadiriwa kufikia milioni nne wakiambukizwa virusi vya HIV kila mwaka.

Katibu mkuu wa umoja wa mataifa Kofi Annan amewataka watu kuendelea na mapambano dhidi ya ukimwi, akiongeza kuwa wanasiasa wanapaswa kuwajibika.

Katika sherehe za maadhimisho hayo mjini New York , Annan amesema kuwa virusi vya ukimwi, ambavyo vimeuwa watu zaidi ya milioni 25 na kuambukiza watu milioni 40 zaidi, ni changamoto kubwa katika enzi zetu.

Eneo la Afrika kusini mwa jangwa la Sahara linabaki kuwa ndio eneo lililoathirika zaidi, likiwa na watu milioni 24.7 walioathirika.