1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Maandamano ya ‘No Kings’ yafanyika kupinga utawala wa Trump

Saleh Mwanamilongo
29 Machi 2026

Maelfu ya waandamanaji walikusanyika kote nchini Marekani katika wimbi la tatu la maandamano ya kupinga utawala wa kifalme yanayojulikana kama “No Kings.”

https://p.dw.com/p/5BKwr
USA, St. Paul 2026 | Picha ya droni ya maandamano ya ‘No Kings’ katika Jumba la Bunge la Jimbo la Minnesota
Miongoni mwa maandamano kadhaa dhidi ya Donald Trump yaliyofanyika Jumamosi nchini Marekani, lile la harakati za ‘No Kings’ huko Washington lilifanyika katika mazingira ya urafiki mkubwa, likichanganyika na maua ya miti ya cherry na tamasha la vipepeo vya karatasiPicha: Erica Dischino/REUTERS

Waandaaji wamesema zaidi ya matukio elfu tatu yalipangwa, yakilenga sera za Trump kuhusu Iran, udhibiti wa uhamiaji, pamoja na kupanda kwa gharama ya maisha.

Katika mji wa St. Paul, waandamanaji walijaza uwanja wa bunge la jimbo la Minnesota, huku baadhi wakibeba bendera za Marekani zilizogeuzwa chini kama ishara ya kutoridhiswa.

Umati mkubwa pia ulikusanyika katika miji mikubwa kama New York, Los Angeles na Washington.

Ikulu ya White House imepuuza maandamano hayo, ikiyaita kazi ya mitandao ya kifedha ya mrengo wa kushoto, madai ambayo pia yameungwa mkono na baadhi ya wanasiasa wa  chama cha Republican.

Hata hivyo, waandalizi wanasema harakati hiyo inaonyesha kuongezeka kwa kutoridhika miongoni mwa Wamarekani kote nchini.