Israel yaua wapiganaji 40 kwenye mahandaki ya Gaza
1 Desemba 2025
Matangazo
Makumi ya wapiganaji wa Hamas wamejificha kwenye mahandaki ya kusini mwa Gaza, chini ya maeneo yanayodhibitiwa na jeshi la Israeli. Kwa siku 40 zilizopita, wanajeshi wamekuwa wakilenga juhudi zao mashariki mwa Rafah, kwa lengo la kuvunja njia za mahandaki zilizobaki katika eneo hilo na kuwaangamiza wanaojificha humo.Vyanzo kadhaa vilivyozungumza na AFP siku ya Alhamisi vimesema kuwa kuwa mazungumzo yanaendelea kuhusu hatima ya wapiganaji waliobaki kwenye mtandao wa handaki kusini mwa Gaza. Na Jumatano, Hamas ilizitaka nchi zinazoshiriki mazungumzo zishinikize Israel kuwaruhusu wapate njia salama ikiwa ni mara ya kwanza kundi hilo la kukiri hadharani hali hiyo.