UchumiKimataifa
Bei ya mafuta yapungua kwa dola 1 kwa pipa
6 Machi 2026
Matangazo
Taarifa za masoko zinaonesha pipa moja la mafuta ghafi sasa linauzwa kwa dola 84.8 za kimarekani kutoka dola 85.1 jana Alhamisi.
Bei hiyo ni pungufu ya karibu dola moja tangu gharama za nishati ya mafuta zilipopanda kwa kasi duniani baada ya Marekani na Israel kuishambulia Iran jumamosi iliyopita.
Katika kupunguza msukosuko Waziri wa Fedha wa Marekani Scott Bessent amesema wameondoa zuio kwa siku 30 na kuiruhusu India kununua mafuta ya Urusi yaliyokwama baharini.
Hatua hiyo imechukuliwa katika wakati usafirishaji mafuta kupitia ujia muhimu wa mlango bahari wa Hormuz umeporomoka kwa asilimia 90 kutokana na mapigamo yanayoendelea.