Zelensky ashangazwa na matamshi ya Trump kuhusu Ukraine
24 Septemba 2025
Matangazo
Akizungumza Jumanne, Trump alisema Ukraine inapaswa kuchukua hatua sasa wakati ambapo Urusi inakabiliwa na matatizo makubwa ya kiuchumi.
Kulingana na Trump, kwa msaada wa Umoja wa Ulaya, Ukraine iko katika nafasi nzuri ya kupambana na kushinda.
Akizungumza baada ya kukutana na Trump pembezoni mwa Hadhara Kuu ya Umoja wa Mataifa, Zelensky amesema kuna maelewano kwamba kiongozi huyo wa Marekani yuko tayari kuhakikisha usalama wa Ukraine baada ya vita kumalizika.
Matamshi hayo ya Trump yanaaashiria mabadiliko makubwa ya msimamo wake ikilinganishwa na ule wa awali.
Mkuu wa Sera za Kigeni wa Umoja wa Ulaya, Kaja Kallas amepongeza mabadiliko ya mtazamo wa Trump katika mzozo wa Urusi na Ukraine.