1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Migogoro

Wasuluhishi wa Iran kujadiliana na Marekani mjini Geneva

25 Februari 2026

Waziri wa mambo ya nje wa Iran Abbas Araghchi pamoja na timu ya wapatanishi wamekwenda Geneva hii leo kabla ya duru ya tatu ya mazungumzo na Marekani Alhamisi 25.02.2025.

https://p.dw.com/p/59P2u
Ujumbe wa Iran ukiongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Araqchi umeelekea Geneva kwa mazungumzo na Marekani.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Abbas AraqchiPicha: Alexander Miridonov/Kommersant Photo/Sipa USA/picture alliance

Rais Donald Trump anayeiongezea shinikizo Iran la kufikia makubaliano, mapema Jumanne alisema kwa mara nyingine kwamba kamwe hataruhusu Iran kuwa na silaha ya nyuklia.

Washington na Tehran tayari wamefanya duru mbili za mazungumzo yanayosimamiwa na Oman na yanayolenga kupata makubaliano kuhusu mipango ya nyuklia ya Iran.

Ujerumani yaisihi Iran kuachana na mpango wa silaha za nyuklia

Katika hatua nyingine, msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya Ujerumani ameiomba Iran kuachana na mipango hiyo ya nyuklia na makombora ya masafa marefu pamoja na kuacha kuvuruga utulivu wa Mashariki ya Kati.