Tanzania: Vyombo vya habari vya kimataifa vizingatie maadili
23 Novemba 2025
Matangazo
Akizungumza na vyombo vya habari katika kituo cha mkutano cha Kimataifa mjini Dar es Salaam, Msigwa amedai kuwa vyombo hivyo vya habari kama CNN, DW, Al Jazeera na BBC vinachapisha taarifa za upande mmoja na baadae kudai kuwa juhudi za kuwatafuta maafisa wa serikali zimefeli.
DW mara zote hufanya kila juhudi kupata maoni ya kila upande.
Madai ya msigwa yamejiri siku chache baada ya chombo cha habari cha Kimataifa CNN kuchapisha makala fupi iliyoonyesha mauaji yaliyotokea wakati na baada ya uchaguzi wa Oktoba 29, uliompa ushindi Rais Samia Suluhu Hassan.
Hata hivyo serikali hiyo imesema bado inachambua na kuhakiki maudhui yaliyomo katika makala hiyo.