1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Antonio Costa, Ursula Von der Leyen wawasili India

25 Januari 2026

Rais wa Baraza la Ulaya Antonio Costa na Rais wa Tume ya Ulaya Ursula von Der Leyen wamewasili nchini India Jumapili wakati ambapo nchi za Umoja wa Uaya na New Delhi zinatarajiwa kutia saini mkataba wa biashara huria.

https://p.dw.com/p/57QHe
New Delhi, India
Viongozi waandamizi wa India wamewasili India kudumisha ushirikiano na kusaini mkataba muhimu wa biashara huriaPicha: Manish Swarup/AP Photo/picture alliance

Costa na rais wa Tume ya Ulaya Ursula von der Leyen ni wageni wakuu wa maadhimisho ya mwaka huu ya Jamhuri ya India katika jiji la New Delhi yatakayofanyika Jumatatu kabla ya mkutano wa kilele wa 16 wa Umoja wa Ulaya na India.

Mkataba mkubwa wa biashara huria kusainiwa Jumanne

Mkutano wenyewe utafanyika Jumanne wiki ijayo ambapo pande hizo mbili zinatarajiwa kusaini mkataba huo, unaoelezewa kuwa mkubwa kuliko mikataba mingine yote.

Mkutano huo utakuwa fursa ya kujenga ushirikiano wa kimkakati kati ya Umoja wa Ulaya na India na unalenga kuimarisha zaidi ushirikiano kwenye sera muhimu.