AU na EU zaahidiana kuendeleza ushirikiano
26 Novemba 2025
Katika taarifa ya pamoja iliyotolewa Jumanne mwishoni mwa mkutano wa kilele uliofanyika Luanda nchini Angola, nchi hizo zimesisitiza dhamira yao katika kushughulikia athari za mabadiliko ya tabianchi, na kukuza matumizi ya nishati jadidifu barani Afrika.
Amani na utatuzi wa mizozo vyatiliwa mkazo
Rais wa Baraza la Ulaya Antonio Costa amesema pande hizo mbili zimetilia pia mkazo umuhimu wa kuitatua mizozo kote duniani amesema, "Tunasisitiza tena msimamo wetu usioyumba katika kupata amani ya kudumu inayozingatia haki Ukraine, katika eneo linalokaliwa kwa mabavu la Palestina, Sudan, Sudan Kusini, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Sahel, Somalia na katika maeneo mengine yenye mizozo kote duniani."
Pande zote za mazungumzo hayo zimesisitiza tena pia dhamira yao ya kudumisha demokrasia, utawala bora, utawala wa sheria, haki za binadamu na uhuru wa vyombo vya habari.