1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rwanda na Ufaransa zafungua ukurasa mpya

25 Februari 2010

Nchini Rwanda,Rais wa Ufaransa Nicolas Sarkozy amewasili mjini Kigali akiwa katika ziara ya kihisitoria nchini humo.Hii ni mara ya kwanza kiongozi wa Ufaransa ameizuru Rwanda tangu mauaji ya halaiki kufanyika mwaka 1994.

https://p.dw.com/p/MAoR
Rais wa Ufaransa Nicolas Sarkozy na mwenzake wa Rwanda Paul KagamePicha: AP

Ziara hiyo inafanyika wakati ambapo Rwanda imeurejesha uhusiano wake wa kidiplomasia na Ufaransa baada ya kuuvunja miaka mitatu iliyopita.Rais Sarkozy anatarajiwa kukutana na mwenzake wa Rwanda Paul Kagame kwa mazungumzo na baada ya hapo watafanya mkutano wa pamoja na waandishi wa habari.Kiongozi huyo wa Ufaransa alikuwa anatokea Mali alikokutana na rais Amadou Toumani Toure.Jee ziara hii ina umuhimu gani kwa Rwanda?

Kigali, Ruanda
Mji Mkuu wa Rwanda,KigaliPicha: DW/Christine Harjes

 Mwandishi:Thelma Mwadzaya

Mhairiri:Mohamed Abdul-Rahman