1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

IS walipataje silaha zao nchini Iraq na Syria ?

Sekione Kitojo
2 Machi 2018

Kundi linalojiita Dola la Kiislamu  kwa kiasi  kibwa limeshindwa. Kiasi ya kilomita za mraba 100,000 zilizokuwa zinadhibitiwa na kundi hilo zimekombolewa. Lakini ilichukua muungano wa mataifa 60 na zaidi ya miaka mitatu.

https://p.dw.com/p/2tZ6d
Syrien Kämpfe um Rakka
mji wa Rakka nchini SyriaPicha: Reuters/Z. Bensemra

Hususan  wakaazi  wa  maeneo  hayo yaliyokombolewa  waliathirika  kwa  kiasi  kikubwa. Watu 10,000 waliuwawa. Mji  mkuu  wa  kundi  hilo  la  IS Rakka  nchini  Syria ni magofu  matupu, kama  ulivyo  mji  wa  Mosul, Ramadi  ama Tikrit  nchini Iraq.

Hali  iliyochukua  muda  mrefu  kwa  IS  kuwapo  katika  maeneo  hayo na  udhibiti  wao  kuulinda kwa  kumwaga  damu, hauhusiani  tu  na itikadi  kali  ya  wafuasi  wake. Muhimu  kabisa  ilikuwa  hali  ya kuendelea  kwa upatikanaji  wa  silaha  kwa  wapiganaji  hao  wa Jihadi.

Syrien Kämpfe um Rakka
Mashambulizi ya anga dhidi ya mji wa Rakka uliokuwa ukidhibitiwa na kundi la ISPicha: Reuters/Z. Bensemra

Sehemu  kubwa  ya  silaha  hizi zinatoka  katika  mataifa  wanachama wa  NATO  barani  Ulaya  na  Umoja  wa  Ulaya, kupitia  Marekani  na Saudi Arabia. Hii  imeelezwa  na  shirika  la  kimataifa la  utafiti  wa silaha  katika  maeneo  yenye  mizozo, katika utafiti  uliofanywa  kwa miaka mitatu.

Watafiti  wa shirika  hilo  walikuwa  katika  maeneo  ya  mapigano  kati ya  julai 2014  na  Novemba 2017.

Walishuhudia  silaha  na  vifaa  vya  kivita , ambavyo wapiganaji  wa muungano  unaopambana  na  kundi  la  IS walikuwa  nazo. Kati  ya Kobane  na  mpaka  kati  ya  Syria  na  Uturuki pamoja  na  mji  mkuu wa  Iraq  Baghdad, wataalamu  wa  shirika  hilo walionesha  kiasi  ya silaha  2000  na  zaidi  ya  risasi 40,000. Na  waliweza  kuonesha ushahidi  wa  namba  za  silaha  hizo  na  njia zilizopitia  hadi  kuwafikia wapiganaji  hao  wa  IS. Nani  aligharamia, kazi  hiyo  ilifanywa  na Umoja  wa  Ulaya  na  wizara  ya  mambo  ya  kigeni  ya  Ujerumani.

Halbautomatische Waffe
Silaha kama hizi ziliwafikia wapiganaji wa IS bila matatizoPicha: picture-alliance/AP Photo/A. Breed

Inashangaza

Damian Spleeters  ni  mkuu  wa  operesheni  wa  shirika  hilo  la  CAR nchini  Syria  na  Iraq na kiongozi  mkuu  wa  ripoti  iliyotokana  na utafiti  huo. Katika  mahojiano  na  shirika  la  utangazaji  la  DW Spleeter  amefafanua , kile  ambacho  kilimshangaza zaidi.

"Kitu kilichonishangaza  sana ni  kwa namna  gani baadhi  ya  silaha zimeweza  kuwafikia IS kwa  haraka  hivyo, mara  tu  baada  ya kuuzwa. Tuna  ripoti inayozungumzia baadhi  ya  silaha  ambazo zimesafirishwa  kuanzia  katikati  ya  Disemba 2016  na  zilikuwa zinatumiwa na  IS  nchini  Iraq, chini  ya  miezi mitatu baada  ya kuuzwa".

Kama  mfano Spleeters  anataja  kombora  la  kupambana  na  vifaru lililotengenezwa  nchini  Bulgaria. Kombora  hilo  liliuzwa  nchini Marekani  Disemba  2015, na  miezi  miwili  baadaye  baada  ya majeshi  ya  Iraq  kuukomboa  mji  wa  Ramadi  kombora  hilo lilipatikana  baada  ya  wapiganaji  wa  IS  kuliacha  wakati  wanakimbia.

Irak Vor einem Jahr überrannte der IS Mossul
Kwa muda wa zaidi ya mwaka mmoja mji wa Mosul ulidhibitiwa na wapiganaji wa ISPicha: picture alliance/dpa/epa/M. Jalil

haifahamika  wazi  iwapo kombora  hilo lilipatikana katika  mapambano na  IS , ama  liliachwa  na  wapiganaji  waliokimbia ama  walilinunua kutoka  katika  makundi  yanayopigana, hilo  bado  halijulikani. Bulgaria ilithibitisha  kwamba  kombora  hilo  liliuzwa  nchini  Marekani.  Komora hilo  la  kupambana  na  vifaru  liliuzwa kwa  kampuni  ya  Marekani  ya Kiesler inayonunua  silaha  kwa  ajili   ya  jeshi la  polisi  la  Marekani. Marekani  hata  hivyo  inasema  haihusiki. Silaha  hizo  hata  hivyo zinafika  katika  eneo  la  Mashariki  ya  Kati.

Mtaalamu  wa  shirika  hilo  la  CAR Spleeters ameona nyaraka  ambazo ni  muhimu  sana, kwamba  Saudi Arabia  na  Marekani  ambazo  ni wanunuzi  wakubwa  wa  silaha  kutoka  Ulaya , hawaheshimu  misingi ya  Umoja  wa  Ulaya  ya  uuzaji  nje  silaha. Na  ndio  sababu  hakuna ufafanuzi   juu  ya  silaha  hizo.

Logo von Amnesty International
Shirika la Amnesty International

Hata  hivyo  huo  ni  nusu  tu  ya  ukweli  Patrick Wilken ana  hakika kwamba  mlolongo  huo  wa  wauzaji  unafahamu  bila  shaka  nani anahusika, kwamba  silaha  hizo  licha  ya  kuwa  na  nyaraka  halisi zilikuwa  zinaelekea  katika  eneo  hilo  la  vita  la  Iraq  na  Syria. Mtaalamu  huyo wa  udhibiti  wa  silaha  wa  shirika  la  Amnesty International  ameiambia  DW ingekuwa kitu cha  ajabu iwapo  mataifa yanayohusika  yasingefahamu  silaha  hizo  zinaelekea  wapi.

Mwandishi:   von Hein, Matthias /ZR/  Sekione  Kitojo

Mhariri: Grace Patricia Kabogo