Makubaliano ya EU-Mercosur kuanza kutekelezwa kwa muda
27 Februari 2026
Utekelezaji huo wa muda umetangazwa kuanza licha ya kuwa bado mahakama ya haki inaendelea kuyatathmini.
Tangazo hilo limetolewa Ijumaa baada ya Uruguay na Argentina kuyaidhinisha makubaliano hayo ingawa tarehe rasmi ya kuanza utekelezaji haijabainishwa. Brazil na Paraguay bado hazijayaidhinisha lakini yanatarajiwa kufanya hivyo hivi karibuni.
Makampuni ya Ulaya, Argentina na Paraguay kuanza kunufaika
Hatua ya Ulaya kuanza kuyatekeleza makubaliano hayo kwa muda inayaruhusu makampuni ya Umoja wa Ulaya, Argentina na Paraguay kunufaika na kanuni mpya za forodha kabla ya makubaliano hayo kuanza kutekelezwa rasmi.
Uamuzi huo hata hivyo umekosolewa vikali na Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron aliyeuita wa kushangaza na kuwa kufanya hivyo kabla ya tathmini ya mahakama ya haki ni tabia mbaya na kumeishtusha Ufaransa.