1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Bunge la Namibia kujadili makubaliano ya fidia ya Ujerumani

Grace Kabogo
22 Septemba 2021

Bunge nchini Namibia kujadili makubaliano kati ya nchi hiyo na Ujerumani kulipa fidia kwa wahanga wa mauaji ya kimbari ya wakati wa ukoloni wa kijerumani ambayo bado hayajasainiwa.

https://p.dw.com/p/40eeE
Namibia Windhoek | Proteste gegen Genozid Abkommen mit Deutschland
Picha: Sakeus Iikela/DW

Majadiliano ya bunge nchini Namibia kuhusu makubaliano kati ya nchi hiyo na Ujerumani kulipa fidia kwa wahanga wa mauaji ya kimbari ya wakati wa ukoloni wa kijerumani ambayo bado hayajasainiwa, yanatarajiwa kuanza tena Jumatano.

Spika wa Bunge, David Nahongandja amesema siku ya Jumatano kuwa ana matumaini kura inaweza ikafanyika katika siku zijazo.

Kura hiyo imecheleweshwa baada ya vikao vya bunge kuahirishwa mwezi Juni kutokana na kuongezeka kwa maambukizi ya virusi vya corona.

Kwa mujibu wa Nahongandja, wabunge wa upinzani mara kwa mara waliizuia serikali kuwasilisha makubaliano hayo bungeni hapo jana.

Takribani watu 300 waliandamana nje ya jengo la bunge kupinga makubaliano yaliyopendekezwa.