Urusi yaapa kuendeleza mashambulizi dhidi ya Ukraine
25 Septemba 2025
Urusi imeapa kuendeleza mashambulizi yake ya kijeshi nchini Ukraine na kupuuzilia mbali madai ya Rais Donald Trump kwamba jeshi la Kiev linaweza kuyarejesha tena maeneo yanayoshikiliwa na vikosi vya Moscow. Rais Trump aliitaja Urusi kuwa chui asiye na meno na kusema anaamini Ukraine inaweza kurejesha kila kipande cha ardhi kilichotekwa na vikosi vya Mosow.
Matamshi ya Trump yalifuatia mazungumzo yake na Rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky kando mwa mkutano wa Umoja wa Mataifa, yalikuwa ni mabadiliko makubwa katika msimamo wake kuhusu mzozo huo wa miaka mitatu na nusu sasa, ambao wakati anaingia madarakani alijigamba kwamba angeumaliza ndani ya saa kadhaa. Jeshi la Urusi linashikilia karibu asilimia 20 ya ardhi ya Ukraine, ikijumuisha rasi ya Crimea iliyonyakuliwa mwaka 2014.