Wanawake wachuuzi wa samaki katika Ziwa Tanganyika nchini Tanzania, wanaendelea kukumbana na unyanyasaji, huku wakitumia miili yao kupata bidhaa za samaki kutoka kwa wavuvi wa ziwa hilo. Hali hiyo pia inaelezwa kuchangia kuenea kwa virusi vya Ukimwi na maambukizi ya magonjwa ya zinaa.