1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Uchumi

Umoja wa Ulaya na Australia zakubaliana mkataba wa biashara

24 Machi 2026

Umoja wa Ulaya na Australia zimefikia mkataba wa biashara huru miaka minane tangu mazungumzo hayo yalipoanza.

https://p.dw.com/p/5Azx1
Australia Canberra 2026 | Von der Leyen na Albanese wasaini mkataba wa biashara huru kati ya EU na Australia
Mkataba wa biashara huru ambao umefikiwa kati ya Umoja wa Ulaya na Australia kuondoa ushuru wa asilimia 99 kwa bidhaa za Umoja wa UlayaPicha: Lukas Coch/AAP/dpa/picture alliance

Umoja wa Ulaya na Australia zimekubaliana kuhusu biashara huru baina yao.

Rais wa halmashauri kuu ya Umoja wa Ulaya Ursula von der Leyen na Waziri Mkuu wa Australia Anthony Albanese, wametangaza hayo siku ya Jumanne, takriban miaka minane tangu mazungumzo hayo ya biashara huru yalipoanza.

Mkataba huo utaondoa zaidi ya asilimia 99 ya ushuru kwenye bidhaa za Umoja wa Ulaya zinazopelekwa Australia kibiashara. Hayo ni kulingana na shirika la habari la AFP.

Australia pia itapunguza ushuru kwa uagizaji wa madini muhimu.