1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Migogoro

Thailand yatangaza amri ya kutokutoka nje

14 Desemba 2025

Thailand imetangaza amri ya kutokutoka nje katika mkoa wake wa kusini mashariki wa Trat wakati mapigano kati ya taifa hilo na Cambodia yakiendelea kusambaa kwenye maeneo ya Pwani kutokana na mzozo wa mpaka.

https://p.dw.com/p/55K0I
Thailand na Cambodia zimeendelea kushambuliana kutokana na mzozo wa mpaka,
Baadhi ya wakaazi wa Thailand wakiwa kwenye makazi ya muda baada ya kuyakimbia makazi yao kutokana na vita Desemba 08.12.2025Picha: Sarot Meksophawannakul/THAI NEWS PIX/AFP/Getty Images

Hayo yanajiri ikiwa ni siku mbili tangu Rais wa Marekani Donald Trump aliposema viongozi wa nchi hizo wamekubali kusitisha mapigano. Viongozi wa Thailand hata hivyo wamesema hakuna makubaliano ya kusitisha vita yaliyofikiwa.

Mtafaruku wazidi maeneo ya mpakani

Thailand na Cambodia zimekuwa zikishambuliana vikali katika maeneo kadhaa ya mpaka wao wenye urefu wa kilomita 817 tangu Jumatatu.

Mapigano hayo yameibuka baada ya utulivu wa muda tangu mapambano makali ya siku tano ya mwezi Julai yaliyokwisha baada ya Marekani na Malaysia kufanya ususulhishi. Tangu mzozo wa awamu hii ulipoibuka kati ya nchi hizo za Asia, wanajeshi 14 wa Thailand na raia 11 wa Cambodia  wameuawa kwa mujibu wa mamlaka za mataifa hayo.