1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Putin amsifu Al Sharaa kwa kurejesha uthabiti Syria

28 Januari 2026

Rais wa Urusi Vladimir Putin amempongeza mwenzake wa Syria Ahmed al-Sharaa kwa kuongeza kasi ya kurejesha uthabiti nchini mwake baada ya wanajeshi kuyakomboa maeneo yaliyokuwa chini ya vikosi vya wapiganaji wa Kikurdi.

https://p.dw.com/p/57cuj
Rais wa Syria Ahmed Al-Sharaa yuko ziarani Urusi
Rais wa Syria Ahmed Al-Sharaa alipokutana na Rais wa Urusi Vladimir Putin nchini Urusi Oktoba 15,2025Picha: Sergei Bobylev/TASS/picture alliance

Putin ametoa pongezi hizo kwa al-Sharaa ambaye yuko ziarani Urusi kwa mara ya pili tangu Bashar al Assad alipong'olewa madarakani. Aidha Rais wa mpito wa Syria kwa upande wake amemshukuru Putin kwa msaada wake katika kuimarisha hali ya Syria na ukanda wote.

Mazungumzo kuhusu kambi za kijeshi za Urusi

Ziara yake Moscow, inalenga kufanya mazungumzo yatakayojikita katika mustakabali wa kambi za kijeshi za Urusi nchini Syria. Kwa Urusi, ni muhimu kuendelea kuwa na kambi za kijeshi katika Pwani ya Syria ili kuendeleza uwepo wa jeshi lake kwenye eneo la Mediterania.