1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroNigeria

Mwenyekiti wa AU akanusha madai ya Trump kuhusu mauaji

13 Novemba 2025

Mwenyekiti wa Halmashauri Kuu ya Umoja wa Afrika, Mahmoud Ali Youssouf, amekanusha vikali madai ya Rais wa Marekani, Donald Trump, kuhusu mauaji ya kimbari dhidi ya Wakristo kaskazini mwa Nigeria.

https://p.dw.com/p/53WDJ
Ethiopia Addis Ababa 2025 | Umoja wa Afrika | Mahmoud Ali Youssouf
Mwenyekiti wa Halmashauri Kuu ya Umoja wa Afrika Mahmoud Ali YoussoufPicha: Amanuel Sileshi/AFP/Getty Images

Akizungumza na waandishi wa habari katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York, Youssouf amesema hakuna ushahidi unaoonyesha kuwa mauaji ya kimbari yamefanyika kaskazini mwa Nigeria.

Mwenyekiti huyo wa Halmashauri Kuu ya Umoja wa Afrika ameeleza kuwa mtu anapaswa kufikiria kwa kina kabla ya kutoa matamko ya aina hiyo, akisisitiza kuwa waathiriwa wengi wa mashambulizi ya kundi la Boko Haram ni Waislamu na wala sio Wakristo.

Mapema mwezi huu, Rais Donald Trump aliiagiza Wizara ya Ulinzi ya Marekani kujiandaa kwa hatua za kijeshi endapo Nigeria itashindwa kukomesha kile alichokitaja kuwa mauaji ya Wakristo. Hata hivyo, hakutoa ushahidi mahsusi kuthibitisha madai hayo.