Mwanaharakati maarufu Jesse Jackson afariki dunia
17 Februari 2026
Matangazo
Mwanaharakati na mwanasiasa wa miaka mingi aliyewahi kugombea mara mbili kiti cha urais nchini Marekani Mchungaji Jesse L Jackson amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 84.
Jesse Jackson aliyefariki nyumbani kwake akiwa amezungukwa na familia yake, anakumbukwa kwa kuongoza kwa miongo kadhaa vuguvugu la harakati za kutetea haki za kiraia nchini Marekani baada ya kuuwawa kwa mwanaharakati Martin Luther King Jr. Viongozi mbalimbali waomboleza kifo cha Winnie Mandela
Jackson aliongoza mihadhara ya dini ya kikristo ndani na nje ya Marekani akipambania watu masikini na waliotengwa kwenye jamii katika masuala ya haki ya kupiga kura na elimu na afya.