Muigizaji wa filamu wa Marekani Chuck Norris afariki
20 Machi 2026
Matangazo
Chuck Norris, muigizaji filamu za kivita wa Marekani na nyota wa Hollywood maarufu kwa uigizaji wake katika "Walker, Texas Ranger," amefariki dunia, akiwa na umri wa miaka 86.
Familia yake imesema katika taarifa kwenye Instagram hivi leo kwamba ni kwa mioyo mizito ambapo wanatangaza kifo cha ghafla cha mpendwa wao Chuck Norris kilichotokea jana asubuhi.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo familia imesema aliishi maisha yake kwa imani, kusudi, na kujitolea bila kuyumba kwa watu aliowapenda. Kupitia kazi yake, nidhamu, na wema, aliwatia moyo mamilioni duniani kote na kuacha athari ya kudumu kwa maisha mengi.
Inaripotiwa Chuck Norris kuwa aliugua Alhamisi katika kisiwa cha Hawaii cha Kauai.