Mahojiano na mgombea urais Zanzibar Dr.Gharib Bilal
22 Juni 2010Matangazo
Wakati kwa upande wa Jamhuri ya Muungano ni Rais wa sasa Jakaya Kikwete, shauku kubwa zaidi ni huko Zanzibar ambako rais wa sasa Amani Karume anamaliza muda wake baada ya mihula miwili kwa mujibu wa katiba.
Tayari wanasiasa wanane wameshachukua fomu akiwemo Makamu wa rais wa Tanzania Dr.Ali Mohamed Shein na aliyekuwa Waziri kiongozi wa Zanzibar Dr.Gharib Bilal ambaye hii ni mara yake ya tatu kuwania kiti hicho, baada ya kufanya hivyo mwaka 2000 na mwaka 2005 kabla ya kutakiwa na viongozi wa ngazi ya juu wa CCM kuondoa jina lake.
Mohamed Abdul-Rahman amezungumza punde na Dr. Bilal na kwanza anaelezea kwanini akaamua kuchukua fomu na kugombea tena safari hii?
Interview :Mohamed Abdul-Rahman/Dr Gharib Bilal
Mpitiaji:Aboubakary Liongo