1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Jeshi la Israel lasema limewaua ‘magaidi’ wanne Rafah

30 Novemba 2025

Jeshi la Israel limesema Jumapili kuwa limewaua Wapalestina wanne iliowataja kuwa magaidi baada ya kutoka kwenye handaki katika mji wa Rafah, kusini mwa Ukanda wa Gaza.

https://p.dw.com/p/54Vg5
Palestina, Rafah 2025 | Wafungwa wa Kipalestina walioachiwa huru warejea Gaza
Usitishaji wa mapigano katika vita vya Ukanda wa Gaza ulianza tarehe 10 Oktoba mwaka huu, lakini toka wakati huo, Wapalestina zaidi ya 350 wameuawa katika eneo hilo pia, askari kadhaa wa Israel wameuawaPicha: Hasan N. H. Alzaanin/Anadolu Agency/IMAGO

Jeshi la Israel limesema Jumapili (30.11.2025) kuwa limewaua Wapalestina wanne iliowataja  kuwa magaidi baada ya kutoka kwenye handaki katika mji wa Rafah, kusini mwa Ukanda wa Gaza.

Operesheni hiyo ilifanywa kwa mwongozo wa Jeshi la Anga la Israel.

Wakati huo huo, Wizara ya Afya ya Gaza imetangaza kuwa idadi ya vifo kutokana na mashambulizi ya Israel imevuka 70,000, baada ya watu 301 kuongezwa kwenye hesabu tangu siku ya Alhamisi.

Taarifa hiyo imesema watu wawili waliuawa katika mashambulizi ya hivi karibuni, wengine wakitambuliwa kutoka kwenye mabaki yaliyokuwa chini ya kifusi.

Huku mashambulizi yakiendelea, Misri inawapa mafunzo mamia ya maafisa wa polisi wa Kipalestina kwa lengo la kuunda kikosi cha usalama baada ya vita. Zaidi ya maafisa 500 wamehitimu mafunzo mjini Cairo, na mafunzo ya miezi miwili yanaendelea kwa mamia zaidi.