1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaMalta

Wahamiaji 46 na miili kadhaa yapatikana Mediterrania

3 Februari 2023

Walinzi wa pwani ya Italia wamewaokoa wahamiaji 46 pamoja na miili ya watu 8 ikiwemo mwanamke mmoja mjamzito

https://p.dw.com/p/4N3Ki
Picha ya maktaba
Picha ya maktabaPicha: Lebanese Army/AP/picture alliance

Ni baada yaboti waliyokuwa wakisafiri kuonekana kwenye eneo la bahari ya kisiwa cha Malta.

Kulingana na shirika la habari la ANSA chombo hicho kilionekana wakati kikikaribia kufika kwenye kisiwa cha Lampedusa kusini mwa Italia.

Ndani yake kulikuwa na wahamiaji hao kutoka mataifa ya Kaskazini mwa Afrika na wengine waliopoteza maisha.

Kila mwaka maelfu ya wahamiaji kutoka Afrika Magharibi na Kaskazini hufanya safari hatari kujaribu kuvuka bahari ya Mediterannia ili kutafuta maisha bora kwenye mataifa ya Ulaya.