1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Von der Leyen: Vita Ukraine vitafadhiliwa na mali za Urusi

28 Oktoba 2025

Rais wa Halmshauri Kuu ya Umoja wa Ulaya Ursula von der Leyen na viongozi wa nchi za Nordic wamesema wana imani ifikiapo Desemba kutafikiwa makubaliano ya kuvifadhili vita Ukraine kwa mali za Urusi zilizofungiwa.

https://p.dw.com/p/52i78
Deutschland Berlin 2025 | EU-Kommissionspräsidentin Ursula von der Leyen beim Berlin Global Dialogue
Picha: Jeremy Knowles/Eventpress/picture alliance

Akizungumza na waandishi wa habari, Von der Leyen aliyehudhuria mkutano wa viongozi wa Nordic huko Stockholm nchini Sweden, amesema kisheria wazo hilo la kuzitumia mali hizo ni wazo zuri. Waziri Mkuu wa Denmark, Mette Frederiksen amesema analiunga mkono kikamilifu wazo hilo.

Mpango huo lakini umepingwa pakubwa na Ubelgiji, ambayo ndiyo inayoshikilia sehemu kubwa ya mali zenye thamani ya yuro bilioni 200 za Urusi zilizofungiwa.

Ubelgiji inahofia athari za kisheria zinazoweza kutokea kutokana na hatua hiyo na usaidizi itakaopata katika kuubeba mzigo.

Pendekezo hilo litawasilishwa na kujadiliwa katika mkutano wa kilele wa Umoja wa Ulaya mwezi Desemba.