Von der Leyen: Vita Ukraine vitafadhiliwa na mali za Urusi
28 Oktoba 2025
Matangazo
Akizungumza na waandishi wa habari, Von der Leyen aliyehudhuria mkutano wa viongozi wa Nordic huko Stockholm nchini Sweden, amesema kisheria wazo hilo la kuzitumia mali hizo ni wazo zuri. Waziri Mkuu wa Denmark, Mette Frederiksen amesema analiunga mkono kikamilifu wazo hilo.
Mpango huo lakini umepingwa pakubwa na Ubelgiji, ambayo ndiyo inayoshikilia sehemu kubwa ya mali zenye thamani ya yuro bilioni 200 za Urusi zilizofungiwa.
Ubelgiji inahofia athari za kisheria zinazoweza kutokea kutokana na hatua hiyo na usaidizi itakaopata katika kuubeba mzigo.
Pendekezo hilo litawasilishwa na kujadiliwa katika mkutano wa kilele wa Umoja wa Ulaya mwezi Desemba.