Umoja wa Ulaya warefusha muda wa vikwazo kwa Sudan
22 Septemba 2025
Matangazo
Vikwazo vilivyorefushwa ni pamoja na kutaifishwa mali za wanaohusika na mgogoro wa Sudan na kunyimwa ruhusa ya kuzitembelea nchi za Umoja wa Ulaya.
Wanaohusika na vikwazo hivyo ni watu kumi na mashirika manane pamoja na kampuni zinazojihusisha na utengenezaji wa silaha na magari ya jeshi la Sudan linaloongozwa na jenerali Abdel-Fattah al-Burhan.
Vikwazo hivyo pia ni kwa kampuni nyingine tatu zinazohusika na ununuaji wa vifaa vya kijeshi kwa ajili ya vikosi vya RSF vinavyoongozwa na Mohamed Hamdan Daglo.