MigogoroAfrika
Ujumbe wa UM wasema hautoondoka mji wa Akobo, Sudan Kusini
10 Machi 2026
Matangazo
Mkuu wa ujumbe huo, Anita Kiki Gbeho amesema wanafanya mawasiliano na upande wa serikali kuu, ile ya jimbo na washikadau wengine kuhusiana na amri hiyo ambayo amesema hawataitii na wataendelea kubakia kwenye mji huo ili kuwalinda raia.
Vikosi vya serikali ya Rais Salva Kiir vinataka kufanya mashambulizi kwenye mji huo ili kuukamata kutoka mikononi mwa wapiganaji wa upinzani wanaomtii aliyekuwa makamu wa rais Riek Machar.
Duru kutoka mji huo ulio kwenye mpaka na Ethiopia zinasema, maelfu ya watu wameukimbia tangu serikali ilipotoa amri ya kuwataka kuuhama.