Migogoro
Watu wanne wameuwawa Lebanon kwa mashambulizi ya Israel
25 Aprili 2026
Matangazo
Kulingana na vyanzo vya kiusalama, mashambulizi mawili yalilenga lori na pikipiki kwenye mji wa Yohmor. Tukio hilo linaibua mashaka mapya kuhusu utekelezaji wa makubaliano ya kuweka chini silaha katika eneo hilo ambalo limekumbwa na mapigano ya mara kwa mara katika miezi ya hivi karibuni.
Israel yadai ilijihami na kitisho cha mashambulizi ya Hezbollah
Jeshi la Israel limesema lilishambulia mifumo ya Hezbollah ya kufyetulia maroketi iliyokuwa tayari kwa mashambulizi katika maeneo matatu kusini mwa Lebanon.
Chini ya makubaliano ya sasa ya kusitisha vita,Israel inaruhusiwa kujilinda dhidi ya mashambulizi ya kupangwa, yanayokaribia kufanywa au yanayoendelea. Hata hivyo inategemewa kujiepusha na mashambulizi mapya yasiyo na kusudi la kujilinda ndani ya Lebanon.