1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroSomalia

Somaliland yakanusha madai kuwa itawahifadhi Wapalestina

2 Januari 2026

Eneo lililojitenga la Somaliland limekanusha madai ya rais wa Somalia kwamba litawachukua Wapalestina waliopewa makazi mapya au kuwa na kambi ya kijeshi ya Israel kwa kubadilishana na Israel kutambua uhuru wake.

https://p.dw.com/p/56E5N
Rais wa Somaliland Abdirahman Mohamed Abdullahi
Eneo lililojitenga la Somaliland limekanusha kwamba litawahifadhi Wapalestina au kuwa na kambi ya kijeshi ya IsraelPicha: Monicah Mwangi/REUTERS

Wiki iliyopita Israel ilikuwa nchi ya kwanza kuitambua Somaliland kama "taifa huru", hatua iliyozusha upinzani kote Somalia. Siku ya Jumatano, Rais wa Somalia Hassan Sheikh Mohamud, akinukuu ripoti za kijasusi, aliambia televisheni ya Al Jazeera kwamba Somaliland imekubali masharti matatu kutoka kwa Israel ambayo ni: kuwahamisha Wapalestina, kujengwa kwa kambi ya kijeshi kwenye Ghuba ya Aden, na kujiunga na Makubaliano ya Abraham ili kurekebisha uhusiano na Israel.

Wizara ya mambo ya nje ya Somaliland ilikataa masharti mawili ya kwanza. Ilisema makubaliano yake na Israel yalikuwa ya kidiplomasia tu. Somaliland ilijitangazia uhuru wake mwaka wa 1991 na imekuwa na utulivu na amani zaidi kuliko sehemu iliyobaki za Somalia ambayo imekumbwa na migogoro. Somaliland ilianzisha uchaguzi wake, sarafu na hata jeshi.