UN yalani kudhulumiwa Wapalestina
17 Machi 2026
Matangazo
Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya haki za binadamu , imelaani hatua ya Israel ya kutanuwa makaazi ya walowezi na kuwaondosha kwenye ardhi yao maelfu ya Wapalestina katika sehemu kubwa ya Ukingo wa Magharibi, katika miezi ya hivi karibuni.
Ofisi hiyo imesema ina wasiwasi kuhusu uwezekano wa kile ilichokiita takasatakasa ya kikabila dhidi ya Wapalestina.Mataifa ya Kiislamu yalaani udhibiti wa Ukingo wa Magharibi
Ripoti hiyo mpya ya ofisi ya haki za binadamu inayoendeshwa na Volker Turk imetazama hali ilivyokuwa kwa kipindi cha mwaka mmoja kuanzia mwishoni mwa mwezi Oktoba na kutahadharisha juu ya kutanuliwa makazi hayo ya walowezi na kuondolewa kwa nguvu kwa zaidi ya Wapalestina 36,000.