Migawanyiko inashuhudiwa nchini Marekani kuhusiana na suala tete la ubaguzi wa rangi na ukatili unaofanywa na polisi dhidi ya watu weusi karibu kila wakati. Tangu kifo cha George Floyd, Marekani imegawika kati ya wanaopaza sauti kulaani ubaguzi na wale wanaojaribu kuwanyamazisha wakosoaji wa mfumo uliopo. Rashid Chilumba amemuuliza Prof. David Monda iwapo Marekani inaweza kumaliza ubaguzi.