1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mmarekani mwengine mweusi apigwa risasi na polisi Marekani

Amina Mjahid12 Aprili 2021

Maandamano yamefanyika katika jimbo la Minnesota nchini Marekani, baada ya mtu mmoja aliyepigwa risasi na polisi kufariki mjini Brooklyn siku ya Jumapili. Tukio hilo limetokea maili kumi kutoka eneo alikouwawa Mmarekani Mweusi George Floyd aliyewekewa goti shingoni mwake kwa muda wa dakika 10 na afisa wa zamani wa polisi Derik Chauvin.

https://p.dw.com/p/3rtZy

Kulingana na polisi wa eneo hilo, Daunte Wright mwenye umri wa miaka 20 alisimamishwa na polisi waliokuwa na waranti ya kumkamata dereva wa gari alilokuwa anaendesha, na walipojaribu kufanya hivyo Daunte alirejea kwenye gari na kutaka kutoroka na ndipo polisi walipompiga risasi. Amina Abubakar amezungumza na Dr. Nicholas Boaz mchambuzi wa masuala ya kisiasa kutoka Marekani kutoa tathmini yake juu ya muaaji hayo.