1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroLebanon

Hezbollah yaionya serikali inayolenga kudhibiti silaha zaidi

14 Januari 2026

Afisa mwandamizi wa kundi la Hezbollah ameionya serikali ya Lebanon kwamba shinikizo zaidi la kulipokonya silaha kundi hilo nchini humo litasababisha machafuko na pengine vita vya wenyewe kwa wenyewe.

https://p.dw.com/p/56nev
Israel yashambulia maeneo ya Lebanon mjini Beirut
Watu wakitizama kifusi kwenye eneo lililoharibiwa baada ya shambulio la Israel huko Tayouneh, katikati ya uhasama unaoendelea kati ya Hezbollah na vikosi vya Israel, Lebanon Novemba 15, 2024.Picha: Mohamed Azakir/REUTERS

Taarifa hii ni kulingana na maoni yaliyosambazwa na kundi hilo lenye silaha leo Jumatano.

Kundi hilo limeahidi kuziweka silaha zote chini ya udhibiti wa serikali, kufuatia makubaliano ya 2024 yaliyomaliza vita vikali kati ya Hezbollah na Israel

Katika mahojiano na chombo cha habari cha serikali ya Urusi RT, afisa mwandamizi wa kisiasa wa Hezbollah Mahmoud Qmati alisema ikiwa watataka pia kudhibiti silaha kwenye eneo la kaskazini itakuwa ni "uhalifu mkubwa zaidi" unaofanywa na serikali.

Hezbollah inasisitiza kwamba makubaliano hayo yanapaswa kutumika tu kwenye eneo la kusini mwa Lebanon linalopakana na Israel na limekataa kusalimisha silaha zake kwenye maeneo mengine.