1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Frayser-Price bingwa wa dunia kwa mara ya nne

30 Septemba 2019

Mashindano ya dunia ya Riadha yanaendelea huko Doha Qatar. Jumapili kulikuwa na fainali ya mbio za mita mia moja kwa wanawake na mwanariadha wa Jamaica Shelly-Ann Frayser-Price alinyakua taji la nne la dunia.

https://p.dw.com/p/3QUQE
Leichtathletik-WM 2019 100 Meter  Siegerin Shelly-Ann Fraser-Pryce
Picha: AFP/J. Samad

Frayser-Price mwenye miaka 32 ambaye hakushiriki mashindano ya mwaka 2017 kwasababu alikuwa mja mzito, alitimka kwa muda wa sekunde 10.71 na kunyakua dhahabu.

Dina Asher-Smith wa Uingereza akaichukua nafasi ya pili na nishani ya shaba ikachukuliwa na Muivory Coast Marie-Josee Ta Lou.

Rekodi ya Usain Bolt ya medali za dhahabu ilivunjwa Jumapili pia na mwanadada wa Marekani Allyson Felix ambaye pia alikuwa anarudi kutoka kwenye likizo ya uzazi.

Timu ya Marekani aliyokuwemo Felix ilishinda dhahabu katika mbio za kupokezana vijiti za mchanganyiko wa wanawake na wanaume kwa wakimbiaji wanne kwa mita mia nne.