1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

WHO Yapunguza Idadi ya Washukiwa wa Ebola Afrika ya Kati

2 Juni 2026

Shirika la Afya Duniani (WHO) limetangaza kupunguza kwa kiasi kikubwa idadi ya visa vinavyoshukiwa kuwa Ebola katika Afrika ya Kati, hadi 116 kutoka zaidi ya 900 iliyotangazwa awali.

https://p.dw.com/p/5Ek9x
DR Kongo, Bunia 2026 | Mkurugenzi Mkuu wa WHO Tedros atembelea kituo cha matibabu cha Ebola
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani, Tedros Adhanom Ghebreyesus, atembelea Bunia, mji mkuu wa Mkoa wa Ituri, kaskazini-mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), tarehe 31 Mei 2026.Picha: Xinhua/picture alliance

WHO imesema hadi Mei 31, jumla ya visa 321 vimethibitishwa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, vikiwemo vifo 48, huku Ugandaikiripoti visa 9 vilivyothibitishwa na kifo kimoja.

Msemaji wa WHO, Christian Lindmeier, alieleza kuwa kupungua kwa visa vinavyoshukiwa kunatokana na uchunguzi zaidi ulioonesha wengi wa wagonjwa walikuwa na magonjwa mengine kama malaria au homa ya uti wa mgongo.

Alisisitiza kuwa mtu yeyote mwenye dalili zinazofanana na Ebola huorodheshwa kama mshukiwa hadi vipimo vitakapothibitisha.

Mlipuko huo ulitangazwa rasmi Mei 15 katika jimbo la Ituri, mashariki mwa DRC, ingawa unaaminika ulikuwepo kabla ya hapo.

Hadi sasa, hakuna chanjo wala tiba maalum ya kirusi cha aina ya Bundibugyo, hivyo juhudi zinaelekezwa zaidi katika kujikinga na kudhibiti maambukizi.