1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUfaransa

Lecornu anusurika kura za kutokuwa na imani bungeni

16 Oktoba 2025

Waziri Mkuu wa Ufaransa Sébastien Lecornu amenusurika siku ya Alhamisi kura mbili za kutokuwa na imani naye bungeni.

https://p.dw.com/p/526xM
Paris 2025 | Waziri Mkuu wa Ufaransa Sébastien Lecornu akiwa bungeni
Waziri Mkuu wa Ufaransa Sébastien Lecornu akiwa bungeni jijini ParisPicha: Benoit Tessier/REUTERS

Siku ya Jumatano, Lecornu alitangaza kusitisha muswada wa mageuzi ya pensheni unaopingwa vikali na watu wengi na ambao ulitakiwa kuongeza umri wa kustaafu kutoka miaka 62 hadi 64, hatua iliyomuwezesha  Lecornu  kupata uungwaji mkono wa chama cha kisoshalisti.

Kunusurika kwa Lecornu na kura hizo za kutokuwa na imani naye, kunaipa fursa serikali yake kuendelea na kazi ngumu ya kujaribu kupitisha bajeti ya mwaka ujao ambayo inajumuisha hatua za kubana matumizi na kodi mpya. Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron  alitishia kulivunja bunge na kuitisha uchaguzi wa Bunge wa mapema iwapo serekali ya Lecornu ingeliangushwa.