1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Watu mashuhuri 225 wataka mataifa tajiri kusaidia masikini

Sekione Kitojo
2 Juni 2020

Zaidi ya watu mashuhuri 225 wa sasa na viongozi wa zamani duniani wameyataka mataifa 20 yenye utajiri mkubwa duniani kukutana kwa dharura kukubaliana mpango wa dola trilioni 2.5 kupambana janga la ugonjwa wa COVID-19.

https://p.dw.com/p/3d7fB
IWF Direktorin Kristalina Georgieva
Picha: AFP/Getty Images/S. Corum

Na pia  watu  hao  mashuhuri  wametaka  mataifa  hayo   tajiri  kuanzisha  ufufuaji  wa  uchumi  kutokana  na  janga   hilo, hususan kwa  mataifa  yanayoendelea  yaliyoathirika  zaidi  na  yale  yenye uchumi  wa  kati. 

James Wolfensohn Weltbank
Rais wa zamani wa benki ya dunia James WolfensohnPicha: AP

Watu  hao  washuhuri wamesema  katika  barua  kwamba  mataifa haya  masikini  na  yenye  uchumi  wa  kati, ambayo  yanawakilisha asilimia  70 ya  idadi  ya  watu  duniani  na  kwa  wastani  theluthi moja  ya  pato  jumla  la  ndani  la  kila  mwaka  GDP, yanataka ichukuliwe  hatua  haraka. Zaidi  ya  mataifa  100 yameliendea shirika  la fedha  ulimwenguni IMF kutaka  msaada, wamesema  watu maarufu,  na  mengi  zaidi  yanatarajiwa  kufanya  hivyo.

Bila  ya  kuchukuliwa  hatua  kutoka  kundi  hilo  la  mataifa  ya G20, watu  hao  mashuhuri duniani  wameonya  kuwa  mdororo  wa uchumi utakaosababishwa na  janga  la  virusi  vya  corona utaongezeka, na  kuathiri uchumi  wa mataifa  yote,"  na   watu duniani  ambao  wametengwa  na  ni  masikini  wataathirika  zaidi.

Ban Ki-moon The Global Commission on Adaptation
Katibu mkuu wa zamani wa Umoja wa mataifa Ban Ki-moonPicha: Getty Images/AFP/G. Baker

Msaada  kwa mataifa  masikini

Wamesema  kuwa  mataifa  ya  G20, kwa  hivi  sasa  yakiongozwa na  Saudi Arabia, yanawakilisha  asilimia 85 ya  pato  jumla  la  ndani la  wastani  na  yana, "uwezo wa kuongoza  juhudi  hizo  za upatikanaji  wa   fedha  katika  kiwango  kinachohitajika."

"Tuawataka viongozi  kuchukua  hatua  mara  moja," barua  yao imesema. Waliotia  saini  ni  pamoja  na  zaidi  ya  viiongozi  wa zamani  duniani 75, washindi  watatu  wa   tuzo  ya  amani  ya Nobel, washindi  wanne wa  nishani  ya  Nobel  katika  fani  ya uchumi, katibu  wa  zamani  wa  Umoja  wa  Mataifa Ban Ki-moon, mfadhili  George Soros,  rais  wa  zamani  wa  benki  kuu  ya  dunia James Wolfensohn,  katibu  mkuu  wa  zamani  wa  NATO Javier Solana pamoja  na  maafisa  kadhaa  wa  zamani  wa  Umoja  wa mataifa pamoja  na  wataalamu  wa  uchumi wa  hivi  sasa  na wazamani,na   wataalamu  wa  masuala  ya  kiutu  na  afya.

Bildergalerie Kosovo Krieg 15 Jahre Solana
Katibu mkuu wa NATO wa zamani Javier SolanaPicha: Robert Vanden Brugge/AFP/Getty Images

Mkutano  wa  kilele wa   mataifa  yenye  uchumi  mkubwa  duniani ulianzishwa  katika  wakati  wa  mzozo  wa  kifedha  mwaka  2008, lakini  viongozi  hao  wamefanya  mkutano  mmoja  kwa  njia  ya vidio  tangu  kuzuka  kwa  janga  la  ugonjwa wa COVID-19 duniani, na  mkutano  wao mwingine unapangwa  kufanyika  mwezi Novemba katika  mji  mkuu  wa  Saudi Arabia, Riayadh.

katibu  mkuu  wa  Umoja  wa  mataifa  Antonio Guterres amewahimiza  viongozi  wa  kundi  la  mataifa  ya  G20  kabla  ya mkutano  huo  mwishoni  mwa  mwezi  Machi kuidhinisha  mpango wa  baada  ya  vita ikiwa  ni  pamoja  na  kichocheo cha  uchumi, kwa kiwango  cha  trilioni  za  dola, kwa  watu  na  biashara  katika mataifa  yanayoendelea  kujaribu  kupambana  na  janga  la  virusi vya  corona.