Kufuatia kauli ya Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai, kumtaka Mkaguzi Mkuu wa Hisabu za Serikali (CAG) Profesa Juma Assad, kwenda mbele ya Kamati ya Maadili ya Bunge, Mohammed Khelef amezungumza na Rais wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika, Wakili Fatma Karume, juu ya msingi wa kisheria wa mamlaka ya bunge kuweza kumuita CAG.