Kamerhe kuondolewa katika nafasi ya Spika wa Bunge la DRC ?
18 Septemba 2025
Matangazo
Kamerhe anakabiliwa na uwezekano huo wa kuondolewa katika wadhifa huo akituhumiwa kwa usimamizi usio na uwazi wa fedha za umma, uongozi mbaya na kupuuza hoja za wabunge wa kitaifa.
Vital Kamerhe na Félix Tshisekedi waliimarisha ushirikiano wao mjini Nairobi walipounda muungano wao kwa ajili ya mabadiliko baada ya kusaliti makubaliano ya Geneva waliyosaini pamoja na viongozi watano wa upinzani, wakimteua Martin Fayulu kama mgombea pekee katika uchaguzi wa rais wa Desemba mwaka 2018.