1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Migogoro

Urusi yakanusha ndege zake kuingia katika anga ya NATO

22 Septemba 2025

Urusi imekanusha tuhuma kuwa ndege zake zimeingia kwenye anga ya Jumuiya ya Kujihami ya NATO. Msemaji wa Ikulu ya Urusi, Dmitry Peskov ameonya kuwa nchi zilizotoa shutuma hizo zinahatarisha mivutano kuongezeka.

https://p.dw.com/p/50uQX
Estonia yadai ndege za Urusi ziliingia kwenye anga yake Ijumaa 19.09.2025
Picha kutoka jeshi la anga la Sweeden ikiionesha ndege ya Urusi MIG-31 ikiwa kwenye eneo la Jumuiya ya Kujihami ya NATOPicha: Forsvarsmakten/AFP

Ijumaa, Estonia ambayo ni mwanachama wa Jumuiya ya NATO ilisema ndege tatu za kijeshi za Urusi ziliingia kwenye anga yake na kudumu  kwa dakika 12 kabla ya kutolewa nje zikisindikizwa na ndege za Jumuiya hiyo.

Urusi kupitia msemaji wake Peskov imesema madai ya Estonia hayana msingi na ni mwendelezo wa sera yake ya kuongeza mivutano na kuanzisha uchokozi. Kwa upande wa NATO, mabalozi wake watafanya mazungumzo Jumanne baada ya Estonia kuitisha majadiliano yanayohusu tukio hilo.