1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

EU, Armenia wakubaliana kuimarisha ushirikiano

5 Mei 2026

Umoja wa Ulaya na Armenia wamefikia makubaliano ya awali yanayolenga kuimarisha ushirikiano. Makubaliano hayo yamepatikana wakati wa mkutano wa kilele mjini Yerevan siku ya Jumanne.

https://p.dw.com/p/5DKFg
Umoja wa Ulaya na Armenia zimekubaliana kuimarisha ushirikiano
Mkutano wa Armenia na Umoja wa Ulaya umefanyika Yerevan 05.05.2026Picha: Dmytro Rusanov/DW

 Rais wa Halmashauri Kuu ya Umoja wa Ulaya Ursula von der Leyen amesema makubaliano hayo yanaashiria hatua mpya ya ushirikiano kati ya pande hizo.

Ushirika wa Armenia na Urusi unasuasua

Armenia imekuwa na uhusiano wa mashaka na mshirika wake wa muda mrefu Urusi katika miaka ya hivi karibuni. Moja ya sababu ni walinda amani wa Urusi kushindwa kuingilia kati mizozo yake na Azerbeijan. Kwa upande wake Umoja wa Ulaya umeahidi kuiunga mkono Armenia, ukiitaja kama mshirika muhimu wa kibiashara.