1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ulaya yashutumiwa kwa unyanyasaji kwa wahamiaji wa Afrika

22 Mei 2024

Umoja wa Ulaya umekiri kuwa katika hali ngumu, baada ya kundi la vyombo vya habari kusema mataifa ya Tunisia, Moroko na Mauritania, yamekuwa yakiendesha vitendo vya unyanyasaji kwa kutumia fedha za Umoja huo.

https://p.dw.com/p/4g9Wk
Tunisia | Kushughulika na wahamiaji
Wahamiaji wa Kiafrika kwenye kambi ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) katika bandari ya kusini ya Tunisia Februari 14, 2022.Picha: Fathi Nasri/AFP/Getty Images

Uchunguzi uliofanywa na kundi hilo linalovijumuisha vyombo vya habari vya Le Monde na The Washington Post, umeutaja Umoja wa Ulaya kushirikiana na mataifa hayo ya kiafrika katika mpango wa uhamishaji wa watu wengi na ukiukwaji wa haki za binadamu.

Ripoti ya vyombo hivyo imesema Ulaya inaunga mkono, inafadhili na kuhusika moja kwa moja na operesheni ya kuwaweka kila mwaka maelfu ya wahamiaji weusi jangwani au katika maeneo yasiokuwa na watu ili kuwazuwiakufika katika mataifa ya Umoja huo. 

Operesheni hizo zinadaiwa kufanywa kutumia  fedha, magari, vifaa, habari za kijasusi na maafisa wa usalama  kutoka Ulaya na Mataifa kadhaa ya Umoja huo. Msemaji wa Halmashauri Kuu ya  Ulaya Eric Mamer alipoulizwa kuhusu ripoti hiyo alisema inatoa hali ngunu na bado uchunguzi unaendelea.