MigogoroMashariki ya Kati
Netanyahu: Nitahakikisha miili ya mateka wote inarejeshwa
16 Oktoba 2025
Matangazo
Chini ya makubaliano ya kusitisha mapigano yaliyosimamiwa na Rais wa Marekani Donald Trump, Hamas iliikabidhi Israel leo jumla ya miili 30 hivyo kufikia idadi jumla ya miili 120 ya mateka .
Miili ya mateka 19 bado haijulikani iliko, huku Hamas ikisema itahitaji vifaa maalum vya kufukua magofu huko Gaza ili kuipata miili hiyo ya mateka iliyosalia. Kundi la kutetea mateka wa Israel limeitaka serikali ya nchi hiyo kuchelewesha hatua zinazofuata za mpango wa amani iwapo Hamas itashindwa kuirejesha miili hiyo.